Notice: file_put_contents(): Write of 271128 bytes failed with errno=28 No space left on device in /opt/frankenphp/design.onmedianet.com/app/src/Arsae/CacheManager.php on line 36
Warning: http_response_code(): Cannot set response code - headers already sent (output started at /opt/frankenphp/design.onmedianet.com/app/src/Arsae/CacheManager.php:36) in /opt/frankenphp/design.onmedianet.com/app/src/Models/Response.php on line 17
Warning: Cannot modify header information - headers already sent by (output started at /opt/frankenphp/design.onmedianet.com/app/src/Arsae/CacheManager.php:36) in /opt/frankenphp/design.onmedianet.com/app/src/Models/Response.php on line 20 WikipediaNenda kwa yaliyomo
Kila mtu anaweza kuhariri makala yoyote, kutoa makosa ya lugha, kutohoa maneno na kuendeleza na kukuza makala, kwa kuandika kwa ufupi au kwa urefu. Tunakushauri ujiandikishe na kufungua akaunti. Angalia Wikipedia:Mwongozo ili ujifunze unavyoweza kuhariri au kusanifisha ukurasa. Usisite kushiriki; kwa sababu huu ni mradi wa ushirikiano, na hautaisha kamwe. Kamusi elezo itaimarika vizuri zaidi kila wakati. Angalia ukurasa wa jumuia, ukurasa wa jamii, na ule wa makala za msingi za kamusi elezo ili kung'amua unaweza kufanya kazi zipi ili kuboresha Wikipedia.
Mwisho wa Ramadhani ni sikukuu ya Idul Fitri (عيد الفطر - ʿīdu ʾl-fiṭr) ambayo ni sherehe ya furaha na kupongezana. Waislamu hutoa zakat (zakatul-fitri زكاة الفطر) na kuswali, baadaye hukutana kwenye karamu.
Kima punju wa Zanzibar (jina la kisayansi: Piliocolobus kirkii) ni spishi ya nyani wekundu wanaopatikana Unguja, kisiwa kikuu cha Funguvisiwa la Zanzibar, karibu na pwani ya Tanzania bara. Pia wanajulikana kama kolobi wekundu wa Kirk kwa jina la Sir John Kirk, Mwingereza mkaazi wa Zanzibar ambaye kwanza aliwaleta kwenye taarifa ya sayansi ya zoolojia. Sasa inaainishwa kama spishi iliyo hatarini kutoweka na katikati ya miaka ya 1990 ilipitishwa kama spishi kuu kwa uhifadhi wa Zanzibar. Idadi yao bado inapungua, na wahifadhi wanajaribu kufanya kazi na serikali za mitaa ili kubuni mkakati mwafaka na madhubuti wa kulinda idadi ya watu na makazi. Changamoto ni pamoja na makazi ya spishi, ambayo ni ya visiwa tu. Aina hiyo imeainishwa tena mara tatu; hapo awali ilikuwa katika jenasi Colobus, kisha katika jenasi Procolobus, na baadaye katika jenasi Piliocolobus.
Takwimu ya Wikipedia ya Kiswahili
Idadi ya makala: 101,951
Idadi ya kurasa zote: 205,022 (pamoja na kurasa za watumiaji, majadiliano, msaada n.k.)
Katika mwezi wa Agosti 2025 wikipedia ya Kiswahili iliangaliwa mara milioni 7.79 hivi, ambayo ni sawa na mara 251,607 kwa siku au mara 10,483 kila saa ambalo ni ongezeko la mara 4.5 ukilinganisha na mwaka 2024 mwezi wa Agosti. Asilimia 52 za wasomaji wetu wako Tanzania, asilimia 13 wako Kenya, asilimia 18 wako Marekani na mnamo asilimia 10 wako Ulaya.
(fungua anwani kwa browser yako, ondoa majina yaliyopo na ingiza jina la makala (hadi makala 10) unayopenda. Unaweza kubadilisha kipindi cha taarifa utakachoona; takwimu kabla ya 2015 hapa)
na makala 100 zilizotazamiwa zaidi "Topviews" kwa kipindi fulani.
(unachagua kati ya makala 100 kwa mwezi au kwa siku)
Kamusi elezo ya Wiki ni kamusi elezo huru iliyo chini ya Shirika Lisilo la Kiserikali la Wikimedia Foundation, ambalo linasimamia miradi mingine mbalimbali ambayo imeorodheshwa hapo chini. Mpaka sasa miradi inayopatikana Kiswahili ni Wikipedia na Wikamusi. Wikitabu imewekwa Kiswahili lakini bado ni tupu. Mengine inapatikana Kiingereza pamoja na lugha tofauti.